Mwenyekiti wa CCM, Raisi Magufuli amekerwa vikali, na na mamlaka zinazohusika na bodii ya maadili nchini, dhidi ya wasanii wanaoimba majukwaani wakiwaa na mavazi ya utupu, kauli hii ameitoa leo juma nne akiwa anafungua mkutano wa jumuia ya wazazi CCM utakaofanyika siku mbili mjini Dodoma .
Raisi Magufuli, amehoji vyombo vya habari wasimamizi wa maadili na taasisi zinazodhibiti kushindwa kudhibiti, maadili ya vijana .
Msingi wa kauli hiyo ilikuwa kumtaka, kiongozi wa jumuia hiyo atakae patikana kwenda kusimamia, vijana na Taifa kwa ujumla .
Raisi magufuli aliwataka wazazi hao kwenda kusimamia maadili ya vijana na watanzania wote .
"Hii ni jumuia ya wazazi lakini, maadili yameanza kupotea na jumuia ipo kwa ajiri ya kukemea, mimi nimekuwa shabiki mzuri wa mziki, wanaovaa utupu ni wanawake wanaume wanacheza wamevaa sanasana wataachia kifua, waz ili waonekane "six pack" lakini wanawake waliowengi wanaachia viungo vyao".
Raisi Magufuli amesema alipofika bila kujali itkadi yoyote, ya vyama kuungana, katika ujenzi na ulinzi wa maadili ya watanzania .
0 comments:
Post a Comment